Social Icons


Jumatatu, 26 Mei 2014

MBUNGE WA KIBAHA MHE. KOKA, AWAHAMASHISHA WALIMU KIBAHA


Mbunge wa Kibaha Mjini Ndugu Silvestre Francis Koka aliamsha hisia za wafanyakazi wa Shirika la Elimu Kibaha, wengi wao wakiwa walimu kwa kutoa historia yake ya maisha kwa jinsi alivyopambana na umasikini mkubwa hadi kufikia kuwa na uwezo mkubwa wa ki biashara alionao sasahivi.
Mheshimiwa huyo, aliyasema hayo wakati wa kufunga mafunzo yaliyofanywa na Taasisi ya Decision Foundation DFL, Yenye makao yake makuu Iringa mjini na yaliyoongozwa na katibu mtendaji wa Taasisi hiyo ndugu Dominic FN Haule.
Akisimulia jinsi familia yake ilivyokuwa masikini, alisema yeye pia ni motto wa mwisho na wa kiume pekee ambaye ameweza kufanya kila jitihada ya kuthubutu kutafuta mawazo ya biashara, na kukumbatia kila fursa iliyokatiza mbale yake na alianza na kuomba kazi ya umeneja wa Mgahawa wa Jeshi la kujenga taifa ambako alikwenda kwa mujibu wa Sheria.
Kazi hiyo ilimpatia hali ya kujiamini ambayo ilipelekea kuja kuomba na kufanikiwa kupata tenda ya kuendesha mgahawa wa kampuni ya mabasi ya Taifa ya wakati huo iliyokuwa ikiitwa KAMATA. Aliipata kazi hiyo kwa songo mbinde sana kwani aliweza kufukuzwa ofisini humo zaidi ya mara tatu kwa kuwa mhusika aliyeombwa amruhusu kuingia kwa meneja alisema wao walikuwa ni watoto na hawakustahili hata kuthubutu kuomba kazi hiyo kwani kwa hakika wasingeliweza.
Baada ya jitihada za muda, Mheshimiwa Koka alisema, alilazimika kwenda nyumbani kwa Meneja wa kampuni hiyo ambayo haipo tena, na alifanikiwa kumuona meneja ambaye aliwapatia kazi hiyo kwa masharti magumu yaliyojumuisha kuwa na mdhamini amaye atakuwa tayari kulipa fidia ya uharibufu au uvunjifu wa mkataba huo kwani bado naye aliwana vijana hao ambao walikuwa watatu kuwa bado ni watoto wadogo waliokuwa wamemaliza kidato cha sita wakati huo na kuhudhuria JKT tu bila uzoefu wowote.
Mheshimiwa Koka alisema, baada ya kufanya kazi hiyo vizuri, ilipelekea yeye kuomba tena kazi ya kulisha wafanyakazi katika viwanda vya TBL kazi ambayo aliweza kuifanya kwa ufanisi na matokeo yake amefanikiwa kupata kazi zingine migodini.
Akielezea tofauti yake na baadhi ya watanzania ambao hawajafanikiwa kiujasiriamali pamoja na jitihada kubwa Mheshimiwa Koka alisema, yeye alikuwa tangu mwanzo ni mtu wa kufuatilia kazi bila kukuta tama, anajali sana ubora wa bidhaa na huwa hakubali kushindwa hata na makampuni ya kimataifa. Pamoja na hayo Mbunge huyo walisema, ili mjasiriamali afanikiwe ni lazima aipende serikali na kuweza kwenda sambamba na serikali kwani hata katika nchi za wenzetu, wajasiriamali wanaofanikiwa kirahisi ni wale wanaozipenda serikali zao, wanaofuata sharia, taratibu na kanuni na mwishowe huishia kwa serikali kuwanyanyua wafanyabiashara wa aina hiyo kutokana na mafanikio yao.
Mheshimiwa koka alitaja mapato yake ya jumla kwa mwezi ambayo ni makubwa sana japo bado hajaridhika kwani anataka kuongeza kiasi cha mapato hayo pamoja na kuwa ameajiri wafanyakazi wa kitanzania wapatao elfu mbili {2000} ambao anawalipia kodi, akiba ya uzeeni na masurufu mengine wakiwemu na waajiriwa wazungu kumi na moja {11}.
Mheshimiwa Koka alisisitiza na kuwaomba watanzania wengine waanze kuiga mfano wake kwa kutojali kuagiza na kuingiza technolojia kutoa nje ikizingatiwa kuwa dunia ya leo ni ya utandawazi na sote tunalazimika kuwa wafanyabiashira wa kimataifa.
Habari zingine za undani zitaandikwa wiki lijalo baada ya mahojiano yenye lengo ya kuwahamasisha wajariamali wa kitanzania kuhusu jinsi ya kufanya vizuri katika harakati za ukombozi binafsi wa ki uchumi.
+255 767 11 1173

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 

IMADS

INSTITUTE OF MANAGEMENT AND DEVELOPMENT
STUDIES- IRINGA

Sample Text

Sample Text

 
Blogger Templates