Social Icons


Featured Posts

Jumatatu, 2 Oktoba 2017

MRADI WA KILIMO BIASHARA KIJIJI CHA KIKUNDI, MOROGORO Greenhouse

MTAMBO WA KUCHIMBA MAJI UKIWA SHAMBANI KIJIJI CHA KIKUNDI

Baada ya masaa matatu maji yalipatikana mita 90 chini

Mwekezaji akifurahia maji

SHAMBA LIKIONEKANA KWA MBALI

Mwekezaji akifurahia maji

Add caption

GREENHOUSE ILIYOJENGWA NA DOKAMAN INTERNATIONA KIKUNGWI ZANZIBAR Sept 2017

Ujenzi wa band la ng'ombe Zanzibar uwezo Lita 15 hadi 20 kwa siku

MNARA WA TENKI LA MAJI UREFUMITA 4.20

Wafanyakazi wakiandaa sehemu ya kuchimba msingi wa Mnara 
Greenhouse Kikungwi Zanzibar      Sept 2017
Kila upande wa shamba kitalu kuna matuta ya mboga

Alhamisi, 26 Juni 2014

WALIMU WA SHULE ZA MSINGI IRINGA MJINI WAFANYA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI

Baadhi ya walimu wa shule za msingi Iringa mjini wamehudhuria mafunzo ya ujasiriamali yaliyotolewa na Taasisi ya Decision Foundation. Walimu hao wamejifunza namna ya kuanzisha na kusimamia biashara, faida za utandawazi katika biashara na harakati za ukombozi wa Taifa la Tanzania. Walimu hao wameazimia kuanzisha umoja wa kibiashara ili waweze kujikomboa ki-uchumi.

Washiriki wa Mafunzo ya Ujasiriamali yaliyotolewa na Decision Foundation Iringa tarehe 25/26/2014

Walimu wakifuatilia mafunzo kwa ya ujasiriamali kwa umakini

Mwl. Meela, Sugara na Annet Ulaya wakifuatilia mafunzo kwa furaha

Ijumaa, 20 Juni 2014

TAMU ZENYE CHUNGU KATIKA UCHIMBAJI MDOGO WA DHAHABU TANZANIA


HAKIKA KUNA TAMU ZENYE CHUNGU NA CHUNGU ZENYE SALAMA KWA WACHIMBAJI WADOGO WA DHAHABU TANZANIA
Sheria za madini nchini pamoja na mambo mengine, haziruhusu mtu kushika, kukutwa au kufanya biashara ya madini yoyote bila ya kuwa na leseni. Sheria hiyo inamruhusu mwekezaji yeyote wa ndani na nchinya nchi, kuomba leseni ya uchimbaji sehemu yeyote kwa mujibu wa sheria na kutoa fidia kwa mali zilizopo juu ya ardhi kwa wote watakaokuwepo katika eneo lililoombewa kibali. Ndiyo maana baadhi ya watanzania hawaielewi vizuri sheria hii itakayoelezewa vizuri hapo chini. Utaratibu huu wa kuchimba dhahabu kienyeji na kuiuza kienyeji ulimkumba mchimbani mmoja huko Nyalugusu, Mkoa wa Geita ambaye alifanikiwa kupata madebe matatu yaliyojaa dhahabu na kukataa fedha badala yake aliwaomba wanunuzi eti wampatie treni {gari moshi}.
Mzee huyo aliyejitamblisha kwa jina la mangida, alisema yeye shida yake ilikuwa apewe treni aimiliki kwani aliipenda sana. Watu walio karibu nae walimwambia mwandishi wa habari hizi kuwa, wanunuzi hawakumwelewa muuzaji huyo na waliamua kumuacha hotelini mwanza na kuelekea huko India. Tukio hili ni la muda mrefu, takribani miaka 40 iliyopita. Picha chini ni Muuzaji huyo wa dhahabu akiwa na mwandishi wa makala hayo bwana Dominick Haule.
Kisheria, mzee huyu angeliweza kukamatwa na kushtakiwa kwa kisa la kukutwa na madini bila ya kuwa na leseni wala kibali. Huenda angelikuwa mchimbaji mwenye leseni, maafisa wa madini wangelimsaidia kuuza madini hayo.
Sheri za madini zina watatanisha sana baadhi ya watanzania hususani wale wenye mashamba yaliyopo maeneo yenye madini. Ukiwa na shamba na hata kama una hati ya kumiliki shamba hilo, sheria inaruhusu utoaji wa leseni shambani kwako ili mwekezaji anayetafuta mali iliyopo chini ya ardhi, aweze kuipata mali hiyo kwa sharti ya kukulipa fidia ya kilichopo juu ya ardhi kwani ardhi ni mali ya serikali. Ni vizuri watanzania wakachukua hatua ya kuzifahamu baadhiya sheria za madini ili waweze nao kuomba leseni za madini kama watahitaji kufanya hivyo badala ya kuishia kulia na kulalamika sana kitu ambacho hakitamsaidia mtanzania wala Taifa kwa ujumla.

Kwa taarifa zaidi, maoni au maswali wasiliana na dominickhaule@gmail.com
Simu: 0767 11 1173.

Bwana Dominick FN Haule {katikati} akimhurumia mzee Mangida {kulia kwake} kwa kupoteza madebe matatu ya dhahabu
Mwandishi wa Makala haya {katikati} akizungumza na mzee Mangida {aliyekaa kushoto} ambae alikataa fedha ili auze dhababu madebe 3 kwa kupewa Trani {Gari moshi}

MAJANGA NA MARAHA YA WACHIMBAJI WADOGO TANZANIA


Mwandishi wa makala haya amebahatika kupata baadhi ya taarifa nyingi za uchimbaji na wachimbaji wadogo ambao baadhi yao huamini kuwa kuna sehemu ya ushirikina inatumika jambo ambalo wataalam wanalipinga vikali. Wachimbaji wadogo wa dhahabu ambao nchini idadi yao inakaribia milioni tatu 3,000,000 wamekuwa na changamoto kubwa tatu: -
i.                Tatizo la Kujaa maji migodi yao (mashapo au shafts}
ii.              Tatizo la Mwamba mgumu wanaoukabili ndani ya mgodi na jinsi ya kuutoa baada ya kuuvuja
iii.             Tatizo la mtaji
Wakati utatuzi wa tatizo au changamoto ya kwanza ni kuitatua kwa kupata pampu za maji zenye uwezo wa kutoa maji haraka wakati uchimbaji unaendelea, tatizo la pili la mwamba linatatuliwa na mashine za kisasa za kupasulia miamba {jack hammers na compressors} ambavyo vyote vinahitaji uwekezaji mkubwa kuzidi uwezo wao. Tatizo la kutoa mwamba au vipande vya mawe na udongo wenye dhahabu linatatuliwa kwa kupata mshine ya kunyanyulia mizigo aina ya {crane} zinye uwezo wa tani moja na kuendelea kwani kwa kutumia ndoo, inawachukua matumizi ya nguvu nyingi na muda mrefu sana. Mashine zingeliwawezesha kutoa kiasi kikubwa cha udongo na mawe kwa muda mfupi na kufanya kazi ya kusaga kwa muda mrafu wakiwa namali ghafi nyingi katika stoo zao.
Kuna faida kubwa pia katika uchimbaji mdogo licha ya kuwa na changamoto mbali mbali kwani kwa mchimbaji aliyejipanga anakuwa na uwezo wa kuzalisha hadi kilo moja kila siku. Mwandishi wa makala haya alitembelea mgodi mmoja wa mchimbaji mdogo ambaye uwezo wake ulikuwani nusu kilo ya dhababu kwa siku. Uwekezaji unaweza kutumia kiasi cha shilingi milioni mia tatu 300,000,000/= kwa wachimbaji wadogo wenye uwezo na wanaofuata utaalamu kwani maafisa madini wana taaluma nzuri ya kushauri masuala ya uchimbaji na kumuwezesha mchimbaji mdogo kufikia uwezo huo. Shilingi milioni mia tatu siyo nyingi ukilinganisha na kiasi cha dhahabu ya nusu kilo kinachopatikana kila siku kwani kiasi hicho kinaweza kuuzwa hadi shilingi milioni 40 {nusu kilo ya dhahabu.
Wito ni kwa watanzania wanaotaka kuwekeza wawasiliane na iMADS ili wapate taarifa kamili na maandiko ya miradi ya jinsi ya kuwekeza katika madini aina ya dhahabu kwani kitengo hiki cha chuo, kina taarifa zote muhimu za kibiashara za uchumbaji wa dhahabu.
Pamoja na maraha ya faida, hiyo huwa ni kwa wawekezaji, lakini kwa upande wa wachimbaji wadogo wana machungu yao kama yalivyoshudiwa na mwandishi wa makala hayo alipotembelea migodi na kujikuta analazimika kusaidia kusimamia shughuli za maafa na majanga katika baadhi ya maeneo. Picha hapo chini zinaonesha wachimbaji wadogo ambao wengi wao hawajajipanga, hawafuati taratibu za usalama na kujiweka muda mwingi hatarini. Wachimbaji waliangukiwa na mgodi, walikaa ndani ya shimo kwa siku tatu na siku ya nne tulifanikiwa kuwatoa wakiwa hoi, bila chakula siku nne, bila maji na hewa kiduchu mno. Walikuwa hawana nguvu na hawakuamini kuwa waliokolowa. Wachimbaji hao wadogo walidai kuwa kama tusingelikuwepo sisi wageni, basi ingelikuwa mwisho wao kwani baadhi ya wachimbai walikuwa na imani potofu kuwa, eti mgodi wenye maafa hutoa dhahabu nyingi {hutapika dhahabu} kitu ambacho siyo cha kweli, kwani wachimbaji wengi wanaofanikiwa ni wale wanaowatumia wataalam ao maafisa wa madini waliobobea katika taaluma zao.
Kwa taarifa zaidi na maelezo au kama una mchango wa mawezo wasiliana na
Dominickhaule@gmail.com Cell Phone: 0767 11 1173

MAJANGA YA WACHIMBAJI WADOGO WA DHAHABU TANZANIA

Wachimbaji wadogo wanye uwezo kiasi, wakiandaa mtambo tayari kwa kazi ya kutoa maji shimoni

Ohooo! Asanteni Jamani. Sauti ya mchimbaji mdogo ilisikika kwa mbali

Askari wa usalama akiwalinda majeruhi na kuhakikisha zoezi linafanyika kwa amani na utulivy

Majeruhi akipelekwa sehemu ya huduma ya kwanza

Mchimbaji mdogo anaeshindwa kulia, akijaribu kushukuru kwa shida huku akipumua kwa tabu

Majeruhi akitolewa shimoni alimokaa siku nne

Mwandishi wa makala haya akisaidia kusimamia  kikamilifu uokoaji

Mmoja ya walionusurika kufa mgodini akiwahishwa kwa huduma ya kwanza

KARAHA NA MARAHA YA WACHIMBAJI WADOGO


Wachimbaji wadogo wa dhahabu wanapata dhahabu kwa namna mbili. Namna ya kwanza ni kama vile wanaokota vipande vya dhahabu ambavyo kwa asilimia kubwa vinabeba dhahabu na vinajulikana kwa jina la vikole {Alluvial Gold}, vipande hivi huweza kufikia 98% ya dhahabu na uchafu ukawa asilimia mbili tu. Asilimia hizo huwasilisha kiwango au kiasi cha dhahabu kilichomo ndani kwa uwiano wa kipande kizima. Kitu cha Ajabu kidogo katika uokotaji huu ni matokeo ya nyakati tofauti yanayofanya aneo Fulani lifurike ghafla dhahabu nyingi za vipande au vikole hasa katika maeneo ya kingo za mito.
Ikitokea sehemu imepata dhahabu ya aina hiyo ambayo mara nyingi ninakuwa ni kama vile imeshushwa ghafla kutoka mbinguni, mtu wa kwanza kuiona na kuiokota kiasi Fulani hata kama ni usiku, huwa haitaji kuwaarifu watu isipokuwa kwa namna ya ajabu, ndani ya siku mbili unaweza kushangaa kuwa watu zaidi ya elfu 20 wanaweza kupatikana sehemu hiyo na isijulikane wamejuaje na wametoka wapi, ni matokeo ya kama vile miujiza. Kitondo cha dhahabu kutokea ghafla huitwa rashi {rush} inaelekea ni wachimbaji wadogo wanatumia neno hilo lenye asili ya kiingereza linalomaanisha watu wengi kwa wakati mmoja kukimbilia sehemu ilikoibuka dhahabu.
Tafiti nyingi zinaonesha kuwa Tanzania ina madini mengi na dhahabu imeenea karibu katika kila wilaya ikitofautiana kwa kiasi na kiwango tu. Wachimbaji wa dhahabu hutumia vifaa duni ambavyo vinashangaza kwa jinsi vinavyoweza kuwafikisha chini hadi kufikia urefu wa futi mia mbili {200} na wanaweza kwenda kulia na kushoto hadi mita zaidi ya futi 200 tena. Wakati mwingine hukutana na wachimbaji wengine ndani kwa ndani na wanaweza kuzua mapambano yenye kuhatarisha maisha. Mashimo kwa juu kama picha zinavyoonesha huwa na size ndogo sana ya hadi mita moja ya mraba.
Mashimo hayo hufungwa mbao au miti {uharibufu wa mazingira} nyingi zinazojulikana kwa jina la kichimbaji kama “Matimba”. Miti hii hufanya kazi ya kuzuia mashimo yasibomoke kirahisi hasa wakati wachimbaji wakiwemo chini ya ardhi. Miongoni mwa  matatizo yanayoweza kutokea chini ya ardhi ni pamoja na ukosefu wa hewa au kufika maeneo yanye hewa yanye sumu na hapo wachimbaji hupoteza maisha. Mchimbaji anakuwa na tochi iliyofungwa kichwani na mpira kwa lengo la kumsaidia mwanga ilia one vizuri. Huwa hawavai vifaa vya usalama kama vile miwani maalum ya kulinda macho, kofia za plastic au chuma na viatu maalum wa usalama ili kuliinda miguu isiumie. Unaweza kutizama picha hapo juu.
Ujenzi wa mashimo au migodi ya wachimbaji wadogo hujumuisha uchimbaji wa shimo lenyewe ukubwa umeandikwa hapo juu, uwekeji wa miti, mbao au zege, uezekaji na matumizi ya vifaa kama kamba na mipira ya kuingizia hewa na mipira ya kutolea maji.
Kwa ushauri, au taarifa zaidi wasiliana kupitia dominickhaule@gmail.com
 

IMADS

INSTITUTE OF MANAGEMENT AND DEVELOPMENT
STUDIES- IRINGA

Sample Text

Sample Text

 
Blogger Templates