Social Icons


Ijumaa, 20 Juni 2014

KARAHA NA MARAHA YA UCHIMBAJI MDOGO WA DHAHABU


Moja ya maeneo yenye fursa nzuri za ujasiriamali ni eneo la uchimbaji mdogo wa dhahabu. Uchimbaji wa dhahabu wa asili, unafanywa na wachimbaji wadogo ambao wengi wao hawajui wala hawataki kizifahamu sheria za madini nchini. iMADS imepata fursa ya kufahamu mambo muhimu ya ki-uwekezaji katika eneo hili ambalo lina chungu zenye tamu.
Imeonekana ni vema kuandika mfululizo wa baadhi ya taarifa za msingi zinazoweza kuwasaidia wachimbaji wadogo, wadau, maafisa wa serikali na wawekezaji wengine watarajiwa wanaopenda kuwekeza katika eneo hili. Baadhi ya taarifa zenye raha zitahuzu namna ya Wachimbaji wenyewe, maeneo ya uchimbaji wa dhahabu, changamoto tatu za uchimbaji, aina za vifaa vya ki-asili na vya kisasa vya uchimaji, kiasi cha dhahabu inayoweza kupatikana kwa siku kwa mchimbaji, jinsi maisha ya uchimbaji yalivyo na hatari zake pamoja na masoko na namna uchimbaji wa dhahabu unavyofanyika na jinsi dhahabu nyingi ilivyokuwa ikiuzwa nje ya nchi bila ya Taifa kupata baadhi ya mapato. Mwisho makala itazungumzia madhara na athari za uuzaji wa dhahabu nje ya nchi bila ya kuihusisha serikali. Kwani mwisho wa siku, kila upande unapoteza faida za mapato ya rasilimali hii. Nchi kama Afrika ya Kusini, Dhahabu ni nyara na mali ya serikali na serikali pamoja na wananchi wanapata manufaa makubwa ya dhahabu kwa kushirikishana.
Makala itaandika pia kuhusu maisha ya ujumla ya wachimbaji wadogo na jinsi walivyo na matumizi mabaya licha ya kufanya kazi inayogharimu maisha yao, katu wengi wao hawajapiga hatua za ki-maendeleo ya ki-uchumi. Fuatilia habari hizi na picha kila siku. Picha ya kwanza hapo chini inamuonesha mchimbaji aliyena furaha akitokea ndani ya shimo ambalo huweza kuishi humo kwa zaidi ya siku saba bila kutoka nje.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 

IMADS

INSTITUTE OF MANAGEMENT AND DEVELOPMENT
STUDIES- IRINGA

Sample Text

Sample Text

 
Blogger Templates