Social Icons


Ijumaa, 20 Juni 2014

KARAHA NA MARAHA YA WACHIMBAJI WADOGO


Wachimbaji wadogo wa dhahabu wanapata dhahabu kwa namna mbili. Namna ya kwanza ni kama vile wanaokota vipande vya dhahabu ambavyo kwa asilimia kubwa vinabeba dhahabu na vinajulikana kwa jina la vikole {Alluvial Gold}, vipande hivi huweza kufikia 98% ya dhahabu na uchafu ukawa asilimia mbili tu. Asilimia hizo huwasilisha kiwango au kiasi cha dhahabu kilichomo ndani kwa uwiano wa kipande kizima. Kitu cha Ajabu kidogo katika uokotaji huu ni matokeo ya nyakati tofauti yanayofanya aneo Fulani lifurike ghafla dhahabu nyingi za vipande au vikole hasa katika maeneo ya kingo za mito.
Ikitokea sehemu imepata dhahabu ya aina hiyo ambayo mara nyingi ninakuwa ni kama vile imeshushwa ghafla kutoka mbinguni, mtu wa kwanza kuiona na kuiokota kiasi Fulani hata kama ni usiku, huwa haitaji kuwaarifu watu isipokuwa kwa namna ya ajabu, ndani ya siku mbili unaweza kushangaa kuwa watu zaidi ya elfu 20 wanaweza kupatikana sehemu hiyo na isijulikane wamejuaje na wametoka wapi, ni matokeo ya kama vile miujiza. Kitondo cha dhahabu kutokea ghafla huitwa rashi {rush} inaelekea ni wachimbaji wadogo wanatumia neno hilo lenye asili ya kiingereza linalomaanisha watu wengi kwa wakati mmoja kukimbilia sehemu ilikoibuka dhahabu.
Tafiti nyingi zinaonesha kuwa Tanzania ina madini mengi na dhahabu imeenea karibu katika kila wilaya ikitofautiana kwa kiasi na kiwango tu. Wachimbaji wa dhahabu hutumia vifaa duni ambavyo vinashangaza kwa jinsi vinavyoweza kuwafikisha chini hadi kufikia urefu wa futi mia mbili {200} na wanaweza kwenda kulia na kushoto hadi mita zaidi ya futi 200 tena. Wakati mwingine hukutana na wachimbaji wengine ndani kwa ndani na wanaweza kuzua mapambano yenye kuhatarisha maisha. Mashimo kwa juu kama picha zinavyoonesha huwa na size ndogo sana ya hadi mita moja ya mraba.
Mashimo hayo hufungwa mbao au miti {uharibufu wa mazingira} nyingi zinazojulikana kwa jina la kichimbaji kama “Matimba”. Miti hii hufanya kazi ya kuzuia mashimo yasibomoke kirahisi hasa wakati wachimbaji wakiwemo chini ya ardhi. Miongoni mwa  matatizo yanayoweza kutokea chini ya ardhi ni pamoja na ukosefu wa hewa au kufika maeneo yanye hewa yanye sumu na hapo wachimbaji hupoteza maisha. Mchimbaji anakuwa na tochi iliyofungwa kichwani na mpira kwa lengo la kumsaidia mwanga ilia one vizuri. Huwa hawavai vifaa vya usalama kama vile miwani maalum ya kulinda macho, kofia za plastic au chuma na viatu maalum wa usalama ili kuliinda miguu isiumie. Unaweza kutizama picha hapo juu.
Ujenzi wa mashimo au migodi ya wachimbaji wadogo hujumuisha uchimbaji wa shimo lenyewe ukubwa umeandikwa hapo juu, uwekeji wa miti, mbao au zege, uezekaji na matumizi ya vifaa kama kamba na mipira ya kuingizia hewa na mipira ya kutolea maji.
Kwa ushauri, au taarifa zaidi wasiliana kupitia dominickhaule@gmail.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 

IMADS

INSTITUTE OF MANAGEMENT AND DEVELOPMENT
STUDIES- IRINGA

Sample Text

Sample Text

 
Blogger Templates